Mwigulu Lameck Nchemba ni mtaalamu wa uchumi wa Tanzania na mwanasiasa wa CCM, ambaye amehudumu kama Mbunge aliyechaguliwa wa Jimbo la Iramba Magharibi tangu mwaka 2010.
Mnamo Novemba 13, 2025, Rais Samia Suluhu alimteua kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, akimrithi Kassim Majaliwa.
Kabla ya uteuzi wake wa sasa, alihudumu kama Waziri wa Fedha na Mipango katika Baraza la Mawaziri la Tanzania tangu 31 Machi 2021.
Nchemba alizaliwa Januari 7, 1975 katika Wilaya ya Iramba, Mkoa wa Singida, Tanzania.
Alisoma Shule ya Msingi Makunda, kisha kuhamia Shule ya Sekondari Iboru kwa ajili ya elimu ya kati.
Alimalizia masomo yake ya A-Level katika Shule ya Sekondari Mazengo, akihitimu mwaka 2000 akiwa na stahiki sawa na Diploma ya Shule ya Sekondari.
Mnamo mwaka 2001 alikubaliwa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akihitimu shahada ya Kwanza ya Uchumi mwaka 2004.
Baadaye alipata Shahada ya Uzamili ya Uchumi mwaka 2006, pia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Baadae alipata Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Uchumi kutoka chuo hicho hicho.
Amechaguliwa kuwa mbunge wa Iramba Magharibi mwaka 2010 na akarudishwa bungeni kwa kipindi cha 2015 – 2020. Kwanza, alihudumu kama naibu waziri wa fedha.
Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015, Rais John Magufuli alimteua kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Mwaka 2016 alibadilishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Japo wizara yake ilihusishwa na changamoto kadhaa, ikiwa ni pamoja na rushwa, matumizi mabaya ya fedha, na ongezeko la ajali barabarani.
Tarehe 2 Mei 2020, aliteuliwa kuwa waziri wa Sheria na Katiba kufuatia kifo cha waziri Augustine Philip Mahiga.
Mnamo 31 Machi 2021, baada ya kuundwa kwa Baraza la Mawaziri la Sita la Tanzania, Dk. Philip Mpango alipandishwa kuwa Makamu wa Rais, na Nchemba akachukua wadhifa wa Waziri wa Fedha na Mipango.
Mnamo 4 Julai 2023, aliendelea kushikilia wadhifa wa Waziri wa Fedha, huku Wizara ya Mipango ikiwekwa chini ya Ofisi ya Rais.
Hatimaye, aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania mnamo 13 Novemba 2025 kufuatia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.