Singer turned politician Robert Kyagulanyi, also known as Bobi Wine speaks during a press conference, held at his home in Magere in the outskirts of Kampala, on July 24, 2019. - Ugandan pop star turned leading opposition figure Bobi Wine on July 24, 2019 officially announced he would take on veteran President Yoweri Museveni in 2021 national elections, challenging President Yoweri Museveni who has been in power for 33 years. (Photo by SUMY SADURNI / AFP)
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, ametangaza kuwa ataitisha maandamano ya nchi nzima ikiwa Rais Yoweri Museveni ataiba kura katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Alhamisi ya wiki hii.
Akizungumza na shirika la habari la AFP nyumbani kwake jijini Kampala jana Jumatatu, Januari 12, 2026, Wine (43) amesema kuwa wananchi hawapaswi kusubiri maelekezo yake pindi watakapoona demokrasia yao inachezewa. Amesema kuwa ingawa anafahamu serikali ya Museveni hujibu malalamiko kwa nguvu na ukatili, anaamini kuwa hata tawala za kidikteta zinaweza kuangushwa na nguvu ya umma.
Aidha, akirejea matukio ya hivi karibuni ambapo Marekani iliingilia kati na kumkamata Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro, Bobi Wine amesema angekaribisha uingiliaji kati wa aina hiyo kutoka kwa Rais Donald Trump ikiwa utasaidia kuikomboa Uganda.
Uchaguzi huu unakuja wakati kukiwa na mivutano ya kisiasa kote Afrika Mashariki, huku vijana wakipinga kuminywa kwa demokrasia na ukosefu wa ajira nchini Kenya, Tanzania na kwingineko.
Mashirika ya kimataifa kama Umoja wa Mataifa na Amnesty International yameishutumu Uganda kwa ukandamizaji, ikiwemo kukamatwa kwa mamia ya wafuasi wa Bobi Wine kuelekea siku ya upigaji kura ambapo watu zaidi ya milioni 20 wamejiandikisha.
Rais Museveni (81), ambaye amekuwa madarakani kwa miongo minne, anatarajiwa na wachambuzi wengi kuendelea kushikilia hatamu kutokana na udhibiti wake mkubwa wa vyombo vya dola na usalama.