Na Shafiru Yusuph- Muleba, KAGERA
Jeshi la Polisi nchini limesema uwepo wa Polisi Jamii imesaidia kupunguza vitendo vya uharifu ambayo imekuwa ikishirikiana na wananchi katika kusimamia usalama wa raia na mali zao.
Kamishina wa Polisi jamii kutoka jeshi la polisi hapa nchini Kamishina wa Polisi Alex Mkama amesema hayo mara baada ya kukutana na Wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa kimilia, wamiliki wa makampuni binafsi ya ulinzi, maafisa watendaji wa mitaa na watendaji wa polisi jamii Mkoani wa Kagera.

Mkama amesema kuwa lengo la kushirikisha jamii ni kupata taarifa sahihi za uharifu na kubaini matishio mapema ya kiusalama hivyo Jeshi la Polisi linatakiwa kubadilika kifikra ikiwemo kushirikisha jamii badala ya kufanya kazi peke yao.
Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera Bravius Chatanda amesema kuwa ushirikishwaji baina ya Jeshi la Polisi na wananchi imesaidia kudhibiti vitendo vya watu kujichukulia sheria mkononi huku vitendo vya watu kutoa ushaidi mahakamani vimeongezeka
