Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Mr Nice amesema msanii TID alitumia umaarufu wake kujijengea nafasi na kuvuma zaidi katika tasnia ya muziki, akidai kuwa si TID pekee bali wasanii wengi walitumia upepo wake kufikia mafanikio.
Akizungumza leo Julai 6 mara baada ya kuwasili nchini akitokea Kenya, Mr Nice amesema amerejea kushiriki tamasha kubwa la 30 ya Bongo Fleva, huku akieleza kuwa anafurahia kukutana tena na mashabiki wake wa Tanzania.
Msanii huyo amesema tamasha hilo litakuwa fursa ya kuwakutanisha wasanii mbalimbali waliotoa mchango mkubwa katika ukuaji wa muziki wa Bongo Fleva na kuwakumbusha mashabiki historia ya muziki huo.
Tamasha la 30 ya Bongo Fleva linatarajiwa kufanyika Julai 10, ambapo mashabiki wanatarajiwa kushuhudia burudani kutoka kwa baadhi ya majina makubwa ya muziki nchini.
