AMINA SEMAGOGWA

Amina Deogratius Semagogwa (SEMA G) ni mwandishi wa habari na mtangazaji mahiri wa Radio mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika tasnia ya habari, Amebobea katika kuandaa na kuendesha vipindi vyenye uzito vinavyolenga kuibua mijadala ya kijamii, hususan katika malezi bora ya watoto na masuala ya utawala bora. Kupitia kalamu na sauti yake Amina ametunukiwa tuzo zaidi ya 10 za uandishi bora wa habari nchini Tanzania , Amina amejijengea nafasi ya kuwa daraja kati ya jamii na maarifa, akiamini kuwa uandishi wa habari si kuripoti tu bali ni chombo cha kuelimisha, kuhamasisha na kuleta mabadiliko chanya, Ana mtindo wa kipekee unaochanganya weledi, uchambuzi na uwasilishaji unaogusa maisha halisi ya watu. Kauli mbiu: Sauti ya jamii, dira ya mabadiliko.